Mmh, mmh Oh yeah yeah yeah yeah yeah yeah Mbio za sakafuni huishia ukingoni sikujua We nenda salama mi najiuguza Wameshakurubuni fadhila zangu huzioni natambua Siwezi kung'ang'ana ushanipunguza Hee ninajihisi bahati sina, sahau yote ya jana Bora ungesema mapema kama kuna kosa nilokutendea Uliniahidi utanilindia heshima, hutaifanya danga Kumbe hata yale maneno mazuri uliyosema uliongopea Ooh Baba! Kumbe siri ya mtungi aijuaye kata Ooh Baba! Moyo umeumbwa kupenda mwingine nitapata Ooh Baba! Yakiisha mavumbi mafua yatakata Ooh Baba! Na ukweli haufungwi kwenye penzi la balaa Sina bahati, sina bahati Sina bahati, sina bahati Nilishajaribu kufosi hadi kupiga ndele (sina bahati) Ila bado nimikosi acha niende mbele Eh sishindani na upepo kwa mbio Limenikosa sikio Mie kichwa nijigeuze kalio Bure nitajiumiza Mizani haipimi kulia Shetani amelibamia Siku hizi anajiita fagio Anawamaliza eeh Mwili wema wangu umeniponza Ni mifupa nono kulifyonza Umeniacha njia panda mi naoza Bila huruma Masikini moyo umenichonza Jahazi lazama ye nahodha Mateso kila likichomoza I wish siku zirudi nyuma Ooh Baba! Kumbe siri ya mtungi aijuaye kata Ooh Baba! Moyo umeumbwa kupenda mwingine nitapata Ooh Baba! Yakiisha mavumbi mafua yatakata Ooh Baba! Na ukweli haufungwi kwenye penzi la balaa Sina bahati, sina bahati Sina bahati, sina bahati Nilishajaribu kufosi hadi kupiga ndele (sina bahati) Ila bado nimikosi acha niende mbele