Hallooo Weweweaah Aah Kutwa viguru njiani majirani wote wamekuchokaa Mara chumba cha fulani mtu gani we kwako usio kaa Washinda vibarazani vya wenzako kuropoka Ukome mwana fulani ona uso ulivyo kukoboka Sio mwisho vibaoni hadi kwenye vigodoro Usio na haya usoni kote wazua migogoro Hivi wee haujioni kuwa una kasoro Usio mchana jioni si wajuzi si tomorrow Sio mwisho vibaooni kwenye vigodoro Usio na haya usoni kote wazua migogoro Hivi wee haujioni kuwa una kasoro Usio mchana jioni si wajuzi si aah Nasema nawe (nasema nawe) Nasema nawe (nasema nawe) Nasema nawe (nasema nawe) Usio haya nasema nawe Umezoea (nasema na wewe) Chezea chezea (nasema nawe) Umezidi (nasema nawe) Zizi, zidi (nimechoka nasema nawe) Huna haya ka kibakuli cha vumba Popote unajitokeza babu eee Haa, we kichoji tu Unaingia kwenye kundi la ninga Utachanika mabawa Hmm ah Zingifuli zingifuli ungezinga mahala ukakaa Usio mila desturi usio jua tongozwa ukakataa Usio hiyana fedhuri uongo umekujaa Kujifanya mashuhuri kumbe chaka umechaka aga Mwenzako mi ni turufu si garasa Mwenye nyota ya umaarufu si kupapasa Tena jokali la nguvu pakarata Lile hodari maguvu si kwasa kwasa Ooh mwenzako mi ni turufu si garasa Mwenye nyota ya umaarufu si hozakoza aah Nasema nawe (ona wewe) Nasema nawe (nawe) Nasema nawe Usio haya nasema nawe Nasema nawe Nasema nawe Nasema nawe Nimechoka nasema nawe Umezoea (nasema na wewe) Chezea chezea (nasema nawe) Umezidi (nasema nawe) Zizi, zidi ooh (usio haya nasema nawe) Nasema nawe (ona wewe) Nasema nawe (ooh) Nasema nawe Nimechoka nasema nawe Wewee umejifunza ngumi leo wataka upigane na Tyson? Haah! Ale kata kata kakata katika si kata Oh teteme teteme (kata) Wenye kusema waseme (kata) Ale kata kata kakata katika si Kata kiuno chako mwenyewe (kata) Mola amekupa wewe (kata) Tena vya kili kilali (kata) Nipe vya bara na pwani (kata) Vile vya nje na ndani (kata) Tumkomeshe fulani (kata) Tena vya kili kilali (kata) Nipe vya bara na pwani (kata) Vya nje na ndani (kata) Akome fulani (kata) Hallo haa Utavunjia ma-apple mwaka huu Maana nazi zimepanda ma bei aah Heheey Toa basi! Ninasema nawe (ona wewe) Nasema nawe (nawe) Nasema nawe Usio haya nasema nawe (wewe) Nasema na wewe Nasema nawe (nawe) Nasema nawe Nimechoka nasema nawe Umezoea (nasema nawe) Chezea chezea (nasema nawe) Ooh nasema nawe Usio haya nasema na wewe (nasema nawe) Nasema na wewe (nasema nawe) Nasema na wewe (nasema nawe) Nasema nawe nimechoka nasema nawe ooh Wewe weah kata kata