Siwema usinipe mateso ya moyo Na sasa nimechoka kweli nasema Siwema usinipe mateso ya moyo Na sasa nimechoka kweli nasema Nilidhani nimepata mpenzi wa kweli Nakumbe nimepatikana na mambo ya ajabu Nia na madhumuni yako nimeshavitambua siwema kaka Siwema kaka, ah, ah, ah Unajitapa mbele ya rafiki zako Kwamba mimi sina la kusema mbele yako Umeniweka kwenye kiganja mama Unalo taka ndilo ninalofanya sababu wewe Ni mzuri sana, siwezi kupata mwengine kama wewe Siwema kaka, unajidang'anya Wema wangu ndio ulioniponza Fadhila zote, kumbe kwako ni bure Malipo yake, kunifanya mjinga Hayo yote, nimakosa yangu Lakini sasa nimejifunza kutokana na makosa Najiepusha nawe mama aaa Nimezunguka Tanzania bara Unguja na pemba nimefika Nimewaona vijana wenye sifa Wenye kujipamba waka pambika Kwa hiyo nielewe brother (Sibabaishwi na sura napenda tabia njema) Sibabaishwi na sura yako (Sibabaishwi na sura napenda tabia njema) Usifikiri mimi rimbukeni sana (Aah na sura napenda tabia njema) Nilikupenda ki mapenzi (Sibabaishwi na sura napenda tabia njema) Ukaniona ni mimi suga mami lako (Sibabaishwi na sura napenda tabia njema) Tabia njema ndio silaha yako (Sibabaishwi na sura napenda tabia njema) Kila mtu atakupenda kaka (Sibabaishwi na sura napenda tabia njema)