Wewe ndiwe Baba Wewe ndiwe Mungu Wewe ndiwe Baba Usikie kilio chao Wengine walia mavazi Wengine walia chakula Wengine walia kulala Wengine walia msaada Wasaidie Eh he, Wasaidie Oh, Wasaidie Eh, Wasaidie Enyi wazazi wa kambo Msiwatese yatima Enyi wazazi wa kambo Msiwatese yatima Nao ni watu, mbele za Mungu Tena wana haki, mbele za Mungu Msiwatese! Wanalia, ye ye ye Eh Mungu, sikia kilio chao! Hawana baba wala mama Ee Bwana, wasaidie Wewe ndiwe msaada wao Ee Bwana, wasaidie Wameumizwa sana na maneno ya watu Wameumizwa sana na maneno ya Walimwengu Ondoa Ondoa uchungu mioyoni mwao Ondoa mawazo mioyoni mwao Ondoa mikwasi mioyoni mwao Ondoa hasira mioyoni mwao Walikula vizuri Leo wala majalalani Walilala pazuri Leo walala mitaroni Mali zao mmechukua ninyi ndugu zao Wakija kuomba chakula, mwawanyima Wakija kuomba Mwawafukuza kama mbwa Kuna siku, watoto Wenu wataitwa yatima Na watateswa kama mlivyowatesa Ee Mungu, watazame yatima Watie nguvu, wasikate tamaa Kuna siku, watoto wenu wataitwa yatima Na watateswa kama mlivyowatesa Wanalia, ye ye ye Eh Mungu, sikia kilio chao! Yesu, naomba unitazame mimi yatima Maana mama ameniacha Walikuwepo nilidhamimiwa sana Lakini kwa sasa, dhamani yangu haipo tena Nisaidie, ewe Yesu Tunapokwenda, wewe ndiwe kimbilio Kwanini mimi, kwanini mimi niitwe yatima?