Nakupenda wewe pekee roho yangu Yakulilia kweli eh njoo kwangu Usiku silali mie nakuwaza we Mawazo nenda rudi yakuzingira we Mapenzi yako kweli yanifaa mimi Maisha bila wewe kweli sijui Mahangaiko yangu yameania patupu Kutoka leo nimeyapiga marufuku Nakupenda wewe pekee Daima mimi na wewe You linger in my mind Hope you're always standing by my side Nakupenda wewe pekee Daima mimi na wewe I have loved you from the start You who holds the key to my heart Nakupenda wewe pekee roho yako Yapendeza kweli yanivuta kwako Upole, ufadhila na ukarimu wa moyo Utu bila uchoyo bali upendo kibao Waliokutangulia hawakushiki Hata wajaribu vipi hawakuwezi Wala sisiti kusema ubaraka kwangu Mvumilivu bila shaka hula bivu Nakupenda wewe pekee sina hofu Maisha yetu pamwe kweli si mabovu Pawe balaa, fununu, chuki na siasa Tukiwa pamoja yote hayo sawa sawa Bahati nzuri tunalo pendo hili Mwenyezi Mungu naye atubariki Tukae pamoja siku nenda siku rudi Katika pendo hili mi na wewe mpenzi