Nani

Ibraah

    Continues after the ad

    (Mocco)

    Asubuhi kumekucha
    Wingu limetanda
    Na mvua yata kunyesha
    Na uko mbali mama

    Maji takitiririka
    Oh baridi itanishika
    We ndo chanda chema
    Uhakika unanikatisha tamaa

    Utaambiwa binadamu
    Ah kila mmoja Ana mapungufu yake
    Sijui nilipoteleza mama

    Si ungeniambia
    Nimemiss tabasamu
    Kutwa kucha
    Picha kummezea mate

    Yangu fimbo umeibeza
    Ah katu hautaki kuitumia

    Labda hesabu za kutoa
    Mi niligawanya baby unisamehe
    Na ile hasi nikafanya chanya
    Baby unisamehe

    Na hata emoji za kulia
    Nazo kutumia nazo zikome
    Japo nipate furaha
    Ah huruma unionee

    Continues after the ad

    Maana hii hali, hata haifichiki
    Kutwa wima cha mpingo, kisiki
    Maana hata nikiona michezo ya njiwa
    Ah huwa naitamani

    Kama si wewe

    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani
    Nani nitampenda

    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani
    Nani nitampenda aah

    Eh penzi usifanye kwa chombo cha usafiri
    Ikawa umeshuka uje utanikatili
    Nitakuwaga mental Niko dhahari
    Si unasikia

    Penzi la dhati daima la wawili
    We fanya na urudi lisiwe batili
    Ka wafanya kusudi ni ukatili
    Mi naumia

    We ndo yangu hifadhi
    Labda nilikosea msimbo
    Kweli kupenda kazi
    Wangu umegeuka fimbo o

    Mi ndo lako koroboi
    Lile lisilo zima
    Aha si ulisemaga hauchomoi
    Kumbe imani ulinipima ah

    Pia ulisema haudonoi
    Wameiteka mazima
    Ahaa simung'unyi sikohoi
    Sina vyangu nimechina

    Maana hii hali, hata haifichiki
    Kutwa wima cha mpingo, kisiki
    Maana hata nikiona michezo ya njiwa
    Ah huwa naitamani

    Kama si wewe

    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani
    Nani nitampenda

    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani?
    Nitampenda nani
    Nani nitampenda aah

    Song details

    Composition:

    Did you see an error?

    Enviar revisão

    Related songs