Limevuja

Mbosso

    Continúa después del anuncio

    Oooh, oooh maya aah
    (Nusder)

    Si umesema mi baniani mbaya
    Na uwepo wangu kwako sio dawa, haya aah
    Penzi nikashona tenzi na riwaya
    Kwenye moyo wako livae liwe sawa, limepwaya

    Napuliza majivu maana moto siuoni
    Kooni maumivu vumbi larudi machoni
    Ahadi za mbivu zimebaki ndotoni
    Lile penzi tulivu leo lipo kikaangoni

    Imeniponza huruma kirungi
    Kujitisha kumsaidia
    Kumbe katoboa mtungi
    Maji yananimwagikia

    Continúa después del anuncio

    Penzi limevuja tena
    Penzi limevuja tena
    Penzi limevuja tena
    Penzi limevuja tena aah

    Ulisema sikiwambaza
    Penzi letu ukuta wa chuma
    Nikitoka kiwalaza
    Utanistiri nywele za nyuma

    Mara kwa mara ulilia
    Kifuani umenilalia
    Ukijuta unayachukia
    Yale ulopitia

    Eti kama mimi hujaona
    Wa kufanana naye
    Asa mbona hukusema
    Kama ushakutana naye

    Napuliza majivu maana moto siuoni
    Kooni maumivu vumbi larudi machoni
    Ahadi za mbivu zimebaki ndotoni
    Lile penzi tulivu leo lipo kikaangoni

    Imeniponza huruma kirungi
    Kujitisha kumsaidia
    Kumbe katoboa mtungi
    Maji yananimwagikia

    Penzi limevuja tena
    Penzi limevuja tena
    Penzi limevuja tena
    Penzi limevuja tena aah

    Información de la canción

    Composición:

    ¿Los datos están equivocados?

    Enviar revisión