Ya Dunia

Serro

    Continúa después del anuncio

    Hayeye!
    Nimesota, sina wera
    Juzi nilikopa nilipe mama mboga
    Hawajui, hawata amini
    Juu mi ni mwana mziki na mambo yangu iko fiti
    Na huko instagrama, wanadhani nimeosa
    Sababu waliona nikikula na Obama

    Wengi ni mastar kwa vile wanavyo vaa
    Lakini utashangaa, vile wanavyokaa
    Wengi hujifanya mambo yao yako sawa
    Lakini utashangaa, ni mengi haya ya dunia

    Hayeye!
    Chakula githeri chemsha na avocado
    Na nina deni ya soo mbili ya mama Wambo
    Sasa nasaka fare anagalau nifike show
    Lakini jana si nilikua kwa TV
    Na juzi pia nilikua kwa gazeti
    Mambo yangu yanafaa kua fiti
    Huko instagrama, wanadhani niko poa
    Sababu waliona, ile poster ya Koroga

    Continúa después del anuncio

    Wengi ni mastar kwa vile wanavyo vaa
    Lakini utashangaa, vile wanavyokaa
    Wengi hujifanya mambo yao yako sawa
    Lakini utashangaa, ni mengi haya ya dunia

    Sio yote yang’aayo ni dhahabu
    Watu huficha masaibu kwa tabasamu
    Basi sote tuwe wakarimu
    Sababu yote yang’aayo si dhahabu

    Wengi ni mastar kwa vile wanavyo vaa
    Lakini utashangaa, vile wanavyokaa
    Wengi hujifanya mambo yao yako sawa
    Lakini utashangaa, ni mengi haya ya dunia

    Información de la canción

    Composición:

    ¿Los datos están equivocados?

    Enviar revisión